BABA
 mzazi wa nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul Juma ‘Diamond’, (pichani) 
Abdul Juma ameibuka ambapo mbali na tukio hilo pia amenena mambo mazito 
kuhusu mwanaye huyo huku akimsukumia tuhuma nzito mama mtu, Amani 
linaanika kila kitu.
ASAKWA PANDE ZOTE ZA DAR
Awali
 lilitangulia zoezi la kumsaka baba Diamond katika pande zote za Jiji la
 Dar es Salaam ili kumsikia alichonacho moyoni kuhusu mafanikio ya 
mwanaye huku taarifa za mahali anapoishi zikipotoshwa na watoa habari 
wetu.
Wapo waliosema mzee huyo anaishi Kibamba, wengine Mbagala, pia wapo waliodai anakaa Manzese au Magomeni, jijini Dar es Salaam.
Timu
 ya mapaparazi wa Amani ilizama kazini kikamilifu ikiapa kumnasa mzazi 
huyo popote alipo na hatimaye Julai 2, 2012 saa saba mchana ilifanikiwa 
kupabamba nyumbani kwake, Magomeni Kagera, jijini Dar es Salaam lakini 
mwenyewe hakuwepo.
Ziliachwa salamu za utambulisho kwa jirani mmoja ili atakaporudi mzee huyo amtaarifu kuwa mapaparazi watarudi siku nyingine.
Julai
 7, 2012 saa tano asubuhi mapaparazi wetu walitinga nyumbani hapo na 
kumkuta mzee huyo akisema alipata salamu na alikuwa akisubiri ujio huo, 
hivyo akawa amejiibua mwenyewe.
AANZA KWA KUANIKA HISTORIA KWA UFUPI
Baada
 ya salamu na utambulisho, mzee huyo alianza kwa kukiri kwamba kweli 
yeye ni baba mzazi wa Nasibu (Diamond) na kuweka wazi kwamba aliachana 
na mama mzazi wa msanii huyo miaka 9 iliyopita.
“Ni
 kweli mimi ndiye Abdul Juma, ni baba mzazi wa Nasibu au Diamond. Eee, 
mimi niliachana na mama Nasibu miaka tisa iliyopita, tena siku 
tunatengana niliondoka nyumbani saa tisa usiku, maana nilikuwa naishi 
kwao (ukweni).
AMGEUKIA DIAMOND
Kinyume
 na matarajio ya kuzungumzia mafanikio ya mwanaye kwa sasa, baada ya 
kuwekwa katikati na waandishi wetu, mzee Abdul ‘aliangusha’ kilio cha 
lawama kwa Diamond kuhusu matendo anayomfanyia kila kukicha.
Mzee
 huyo anayeonekana ‘kisharobaro’ alisema mafanikio makubwa aliyonayo 
mwanaye yasimfanye ashindwe kumthamini yeye kama baba na mapenzi yake 
kuyaelekeza kwa mama yake tu.
“Kuhusu
 Diamond, labda nimwambie huyu mtoto kuwa, amepata mafanikio ndiyo, 
lakini mafanikio hayo yasimfanye ashindwe kunithamini mimi kama baba 
yake na kupeleka mapenzi yote kwa mama yake tu,” alisema.
NI KWANINI?
“Nasema
 hivyo kwa sababu, zamani kabla jina lake halijawa kubwa, mawasiliano 
yetu yalikuwa mazuri sana, lakini nikaja kushangaa baada ya kuwa staa, 
akakata mawasiliano na mimi baba yake, aliangalie hilo.”
Akaongeza: “Sisemi kwa sababu nataka awe ananiletea hizo fedha zake, la hasha! Ila mimi kama baba yake ajue kuniheshimu.
“Diamond
 nampigia simu hapokei, namtumia meseji hajibu, maana yake nini? 
Naumizwa sana na kitendo cha kutopokea simu yangu kila ninapompigia 
kumjulia hali. Na hali hii ameanza mara baada ya kupata mafanikio.
JARIBIO
 LAIVU Katika kuthibitisha hilo, paparazi wetu alimtaka mzee huyo 
kumwendea hewani mwanaye ili kujiridhisha kama kweli ‘hapokeagi’ simu 
yake, simu ikapigwa, ikaita wee mpaka ikakatika.
Baba Diamond: “Si umeona, si nilikwambia ukawa huamini.”
MARA YA MWISHO KUMUONA DIAMOND
Mzee
 huyo aliendelea kutiririka kuwa, mara ya mwisho Diamond kufika nyumbani
 kwake ilikuwa mwezi wa tatu (Machi) mwaka huu baada ya hapo mawasiliano
 yakakatika.
“Diamond
 alikuja nyumbani kwangu mwezi wa tatu ikiwa ni mfungo wa tatu katika 
dini yetu ya Kiislam, akanipa fedha. Baada ya hapo hatujaonana tena wala
 hanijulii hali,” alilalama mzee wa watu.
SMS YA MWISHO KUIJIBU
Alisema
 Aprili, mwaka huu, Diamond alipotwaa tuzo tatu za Kili Music Awards 
2012, yeye alimtumia ujumbe mfupi wa maneno akimpa hongera naye akajibu 
asante baba. Lakini baada ya hapo ikawa imetoka.
“Baada
 ya kufanikiwa kutwaa tuzo za Kili, mwaka huu nilimpigia simu mwanangu 
ili nimpongeze, hakupokea, nikamtumia SMS ndipo akajibu, ‘asante baba’, 
mchezo ukaishia hapo.
“Namshukuru
 sana dada yake, Mwajuma Abdul (Queen Darleen) yeye ndiyo yupo karibu 
sana na mimi kwani mara kwa mara anakuja kunitembelea na wakati mwingine
 hunikumbuka kwa fedha, hata pale aliposhinda tuzo ya Wimbo Bora wa 
Dancehall alifika nyumbani kunionesha tuzo yake, binafsi nilijisikia 
furaha,” alisema mzee Abdul ambaye kwa sasa hana mke.
HAJUI ANAPOISHI MWANAYE
Mbali na msanii huyo kutopokea simu ya baba yake kila anapompigia, vile vile mzee huyo alidai hajamuonesha wapi anapoishi.
“Huyu
 mtoto hajawahi kunionesha anapoishi, sijui anafikiri nikiwa karibu naye
 nitakuwa namuomba fedha. Mimi sina njaa ‘kihivyo’ na wala sitaki fedha 
zake, ila ninachotaka salamu tu, nasikiasikia anaishi Mwenge (usahihi ni
 Sinza Mori) lakini hataki kunionesha.
“Ninachojua
 yote haya yana mwisho kwani nyota aliyonayo sasa kuna siku itazima. 
Simuombei mabaya lakini inaniuma sana kunifanyia hivyo.”
DIAMOND APIGIWA SIMU MARA KUMI NA MBILI
Baada
 ya kupata matamshi hayo ya baba mzazi wa Diamond, mwandishi wetu siku 
ya Jumanne alifanya jitihada za kumpata msanii huyo ili ajibu 
‘mashitaka’ hayo lakini licha ya kupigiwa simu mara kumi na mbili 
hakupokea.
Mbali
 na kupigiwa simu, paparazi wetu alimtumia ujumbe mfupi wa maneno 
kupitia simu yake ya mkononi, lakini pia hakujibu kitu. Juhudi za 
kumsaka zinaendelea.
Source: GPL

 
 
No comments:
Post a Comment