AY 
 HERMY B
"Ningependa
  kujibu shutuma zilizoandikwa  kuhusu uhusiano wangu na  swahiba wangu 
A.Y. Ningependa ifahamike kwamba mimi na A.Y  kwa kipindi  cha miaka 4 
tumefanya kazi za muziki kwa karibu pamoja na kazi nyingine  za 
biashara.  Ni kawaida na inaeleweka kwamba mahali popote watu  
wanapofanya kazi pamoja kugongana katika mawazo au lugha ni jambo la  
kawaida, na ndio changamoto zenyewe. Si jambo la ajabu kama mimi na  
swahiba wangu A.Y. kupishana katika kazi.
Hivyo 
  nimeona ni lazima nijibu kwani nikiiacha bila kujibu madhara yake  
yatakuwa  mabaya.  Kwanza napenda ieleweke sijawahi kuwa msimamizi wa 
kazi  za A.Y zaidi ya kuwa producer wa nyimbo zake tu. Kipindi chote 
hicho  nimekua natumia utaalamu wangu kwenye kutengeneza tu muziki wake.
  Maswala mengine yoooote amekuwa akifanya mwenyewe tena bila msaidizi. 
Pia
 bila A.Y na MwanaFA kunipa nafasi kutengeneza muziki wao  nisingekua 
hapa nilipo. Nadhani inaeleweka mahali popote duniani kwamba  kipaji ili
 kifahamike kwa watu lazima kipitie kwa mtu fulani au mkondo  fulani. Si
 ajabu kama kipaji changu cha kuproduce muziki kimeweza  kufahamika kwa 
kupitia kwa A.Y. Mimi sio mungu labda ningekua sehemu  nyingine na 
mafanikio makubwa zaidi au machache zaidi,lakini nachojua  rafiki yangu 
amenipa ngazi ya kufika huku nilipo sasa, sijawahi kuficha  hilo na hata
 wao wenyewe wanajua na bado nashukuru kwa hilo. 
A.Y
  hajawahi kuingia mkataba wa aina yoyote na kampuni ya BHits Music 
Group  Limited wala mimi binafsi uliombana kufanya kazi na mimi na sio 
mtu  mwingine yoyote. Nimetengeneza nyimbo zisizopungua 30 za A.Y, kwa 
ajili  ya albamu yake katika kipindi cha mwaka 2008 mpaka 2011. Baadhi 
ya  nyimbo hizo zimeshatoka na nyingine bado zipo zikisubiri uhitaji 
wake.  Wote tulikua na lengo la kutengeneza muziki kwa wingi na kuuza 
kwenye  soko zuri la muziki ili tufaidike kwa pamoja. 
Muda
  wote muziki ulikua unatolewa na unafanya vizuri kwa radio na T.V na  
show zilikua zinafanyika na zote nilikua nazijua iwe ndani ya nchi au  
nje ya nchi hii  hata malipo nilikua nafahamu ni kiasi gani na sijawahi 
 kufichwa na A.Y kuhusu hilo. 
Kutoelewana 
 kwetu kibiashara ilikuwa mwezi February mwaka huu yakihusu malipo  ya 
album hiyo. Baada ya hapo niliamua kufunga mdomo wangu na  nisingesema 
chochote kwani haya yalikua yananihusu mimi na rafiki yangu  tu. 
Nimeamua kuongea sasa kwani nahisi nimeshambuliwa kwa mara ya pili  
kuhusu makubaliano haya na mara ya kwanza niliamua kukaa kimya. 
Kwanza
  nataka mfahamu Katika kipindi cha kutokea 2008 mpaka leo hii (miaka 4)
  kwa matumizi ya nyimbo hizo, ambazo amekwishafanyia show nje na ndani 
ya  nchi na nyingine kumpatia nominations na tuzo tofauti, nilichowahi  
kulipwa hakitaweza kuzidi shilingi milioni tatu kwa malipo ya awamu  
tofauti kwa miaka minne.
Kilichotokea
  ni kwamba, mwaka huu mwanzoni kabisa, A.Y aliwasiliana na mimi akiwa 
na  mipango ya kuzindua albamu yake. Na alitaka kuzinunua zile nyimbo  
kutoka kwangu akiwa na mpango mpya wa kuiuza albamu kwa mpango wake  
binafsi pasi na mimi. Nilishindwa kuelewa nini anakifanya hasa alipoomba
  alipie wimbo mmoja mmoja tena kwa bei ya msanii wa kawaida 
anaehangaika  kutoka. 
Niliamua
  kukubali kwamba ameamua kufanya hivyo na sina nguvu ya kumzuia basi  
nikajaribu kupata malipo halisi ya kazi yangu. Ubishi wangu ulikua  
kwamba msanii mdogo hawezi kulipa bei sawa ya kurekodi na msanii mkubwa,
  kwani hata malipo ya msanii mkubwa na mdogo baada ya kazi yoyote iwe 
ya  matangazo ama show huwa hayafanani. Bei niliyotaja haikua millioni  
kumi, ni uongo mtupu na kwa wimbo mmoja niliomba nilipwe millioni 2. 
Akakubali
  kwa bei hiyo ya Millioni 2 japo nilihisi hakuridhika kabisa. 
Nilimtumia  mkataba wa makubaliano yetu ambayo kweli baadae aliona 
kwamba bei hiyo  kwake ni kubwa sana hivyo hatukusaini makubaliano. 
Tulibadilishana  meseji kwa simu kwa muda mrefu sana na niliona biashara
 hii itavunja  urafiki wetu.
Nilifikiria
  sana kwamba nyimbo hizi nimekaa nazo toka 2008 bila kuingiza chochote 
 na maisha yanaenda pia. Sikuona sababu ya kuharibu urafiki wetu wa muda
  mrefu kwa mabishano haya. Kwa Ujumbe wa simu nilimueleza A.Y  
anakaribishwa aje achukue nyimbo zoooooote anazohitaji kwa albamu yake  
BURE (bila malipo).Lakini nilimuomba anisamehe sitomix zile ambazo bado 
 hazijamixiwa, ila ampatie producer mwingine amfanyie hiyo kazi.
Mpaka 
 hii makala A.Y hajaja kuchukua hizo nyimbo na ndio naelewa kua  hayupo 
na BHits tena na wala taarifa zote hizo mbili hajawahi kunipatia.  Huu 
ndio ukweli halisi.
Swala
  la mimi kuwa na wivu na kinyongo na mafanikio ya A.Y ni uongo na  
nashangaa umetoka wapi . Kama kulipwa kidogo, huku nikiona A.Y  
anaingiza fedha nyingi kwa muziki tunaotengeneza pamoja basi ningekua  
nimegombana nae toka mwaka 2009 labda
Narudia
  kwamba nilikua najua kila show yake inapofanywa na sikuwahi kujisikia 
 vibaya. Nataka utambue pia nilikua na akili timamu wakati nafanya kazi 
 na A.Y na muda wowote nilikua na uwezo wa kubadili mawazo na kutaka  
tuandike makubaliano kwa karatasi ila sikufanya hivyo na wala sijutii  
chochote kwa utaratibu wetu wa hatari wa kufanya kazi bila mkataba wa  
maandishi na ndio maana nipo radhi hata sasa kumpatia nyimbo hizo bure  
kama nlivomwambia hapo mwanzo 
Nina
  meseji zote na email za mazungumzo yetu ambazo nilihifadhi nikijua ipo
  siku nitaonekana mimi ndie mkorofi, hivyo nachokisema nina hakika 
nacho  asilimia 100
Picha
  nyingine mbaya ulioichora ni kujaribu kuonyesha kuna kutopendana kati 
 ya maproducer. Mimi Master Jay na Marco Chali ni marafiki wazuri tu na 
 mpaka leo hii nikiwa na shida na nikamhitaji Marco Chali au Master Jay 
 nitampigia simu bila aibu kwani hakuna ugomvi kati yetu. A.Y, Master 
Jay  na Marco Chali pia ni marafiki wa siku nyingi na katika kipindi cha
  miaka minne akiwa Bhits kwa hiari yake na sio mkataba, A.Y amekuwa  
akienda MJ records anapojiskia na mara kadhaa mimi nimeenda na A.Y na  
mara kadhaa nimeenda peke yangu tena kwa ajili ya shughuli zangu  
binafsi. 
Pia
  ufahamu katika kipindi hicho A.Y alikua akitumia muda mwingi MJ 
Records  kuliko Bhits na hiyo yote ilikua ni mipango yake binafsi. A.Y 
hajawahi  kuzuiwa kufanya kazi na mtu mwingine kwani ni msanii huru.
Ndugu
  yangu mimi ni mtu mpole nisiye na ugomvi na mtu hapa mjini. Nasikitika
  sana kwa jinsi kwenye makala yako ulivyojitahidi kuonyesha kwamba mimi
  na swahiba wangu tumejenga uadui. 


 
 
No comments:
Post a Comment