Na James Magai
 
MAWAKILI
 wanaomtetea mwigizaji wa filamu, Elizabeth Michael maarufu kwa jina la 
Lulu anayekabiliwa na kesi ya mauaji, wamewasilisha Mahakama Kuu, Kanda 
ya Dar es Salaam maombi ya uchunguzi wa umri wa mteja wao.
 
Lulu
 anakabiliwa na kesi ya mauaji ya msanii mwenzake Steven Kanumba katika 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, akidaiwa kutenda kosa hilo nyumbani kwa
 marehemu Machi 7, mwaka huu.
Mawakili
 hao waliwasilisha maombi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Mei 7,
 mwaka huu wakiiomba iamuru kesi ya msanii huyo isikilizwe katika 
mahakama za watoto wakidai kuwa mteja wao ni mtoto.
Hata
 hivyo, mawakili hao waligonga mwamba baada ya mahakama hiyo kutupilia 
mbali ombi hilo ikisema ingawa kesi bado iko katika hatua za awali, 
haiwezi kufanya uchunguzi huo kwa kuwa haina uwezo wa kusikiliza kesi 
hiyo.
 
Jana,
 mawakili wanaomtetea msanii huyo waliwasilisha maombi Mahakama Kuu 
wakiiomba itoe uamuzi kama Mahakama ya Kisutu ina uwezo wa kuamua 
ufanyike uchunguzi wa umri halali wa msanii huyo kwa kuwa wanaamini kuwa
 ina mamlaka hayo.
Katika
 maombi hayo namba 46 ya mwaka 2012, yaliyosilishwa na Wakili Peter 
Kibatala kwa niaba ya jopo la mawakili hao, pia wanaiomba Mahakama Kuu 
kama itaridhika kuwa Mahakama ya Kisutu haina uwezo huo, basi yenyewe 
ifanye uchunguzi huo.
Akifafanua
 juu ya maombi hayo, Kibatala ambaye pia ni Makamu wa Rais wa Chama cha 
Wanasheria Tanganyika (TLS), alisema Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009, 
Kifungu cha 113 inaruhusu Mahakama kufanya uchunguzi wa umri wa 
mshtakiwa.
Wakili
 Kibatala alisema lengo la uchunguzi huo ni  kuifanya ijiridhishe kama 
mshtakiwa ni mtoto au ni mtu mzima kwa lengo la kuangalia maslahi ya 
mtoto.
“Baada
 ya uchunguzi huo, mahakama ikijiridhisha kuwa ni mtoto, basi mwenendo 
wa kesi hiyo utaendeshwa kwa maslahi ya mtoto kwa mujibu wa Kifungu cha 
4(2) cha Sheria ya Mtoto,” alisema.
Alisema kifungu hicho huelezea ulinzi na maslahi ya mtoto katika uendeshaji wa kesi kwa watoto wanaokinzana na sheria.
Alisema kifungu hicho huelezea ulinzi na maslahi ya mtoto katika uendeshaji wa kesi kwa watoto wanaokinzana na sheria.
Mawakili
 hao wakiwa katika Mahakama ya Kisutu, walidai kwamba msanii huyo ana 
umri wa miaka 17 na kwa maana hiyo bado ni mtoto na kesi yake haipaswi 
kusikilizwa katika mahakama za kawaida kama mtu mzima.
Katika uamuzi wake, Hakimu Mkazi Augustina Mmbando anayesikiliza kesi hiyo alisema bado iko kwenye upelelezi na kwamba kulingana na jinsi ilivyo isingekuwa busara kuamua hoja yoyote na aliutaka upande wa utetezi uwasilishe maombi hayo kupitia Mahakama Kuu.
Katika uamuzi wake, Hakimu Mkazi Augustina Mmbando anayesikiliza kesi hiyo alisema bado iko kwenye upelelezi na kwamba kulingana na jinsi ilivyo isingekuwa busara kuamua hoja yoyote na aliutaka upande wa utetezi uwasilishe maombi hayo kupitia Mahakama Kuu.
Wakati
 akiwasilisha maombi hayo awali Mahakama ya Kisutu, kiongozi wa jopo la 
mawakili wanaomtetea msanii huyo, Wakili Kennedy Fungamtama alidai kuwa 
mteja wao ana umri wa miaka 17 na si 18 kama inavyotamkwa mahakamani.
Alidai
 kuwa hata cheti cha kuzaliwa walichokiwasilisha mahakamani, kinaonyesha
 mahali na tarehe aliyozaliwa mshtakiwa hivyo kuwa na umri wa miaka 17.
Fungamtama
 alidai kuwa kulingana na Sheria ya Mtoto ya 2009, inatafsiri kuwa mtoto
 ni yule aliye na umri chini ya miaka 18 hivyo katika suala la mteja 
wao, alipaswa kushtakiwa katika mahakama ya watoto.
Hata hivyo,.... Soma zaidi; http://www.mwananchi.co.tz

 
 
No comments:
Post a Comment