KALI YA LEO: BOBAN ASAFIRI KWENDA SUDAN AKIVAA KANDAMBILI
| Haruna Moshi Boban akiwa ndani ya kandambili uwanja wa taifa jana. | 
Kiungo
 mshambuliaji wa timu ya Simba, Haruna Moshi ‘Boban’ jana alikuwa  
kivutio kwa mashabiki, wasindikizaji na hata baadhi ya wasafiri  
waliomuona wakati wakiondoka kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa  
Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam, kuelekea Sudan. 
    
 Simba inakwenda Sudan katika mchezo wa marudiano dhidi ya Al Ahli 
Shandy  utakaopigwa Jumapili ya tarehe 13, mei, 2012 huku ikiwa na mtaji wa ushindi wa mabao 
3-0,  iliyoupata kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.  Uvaaji wa
 Boban, ndio uliowavutia watu kumtizama, kutokana na kuvaa kama  mtu 
asiyesafiri. 
  
 Boban alikuwa amevaa fulana, suruali ya kimichezo ‘trakisuti’ na  
kandambili, hivyo kusababisha watu kuvutika kumuangalia, huku baadhi yao
  wakibaki kujiuliza kuhusu vituko vya nyota huyo ambaye mashabiki  
humuita Balotteli wa Bongo.
 Mchezaji
 huyo anafananishwa na mshambuliaji mahiri wa Italia,  anayekipiga klabu
 ya Manchester City ya England, ambako mara kwa mara  amekuwa akibeba 
vichwa vya habari katika magazeti ya England na Ulaya  kutokana na 
vituko vyake. 
Ukiondoa
 vituko hivyo vya uvaaji wa Boban, msafara wa watu 25 wakiwamo  viongozi
 watano na wachezaji 20 wa timu hiyo waliondoka chini ya uongozi  wa 
mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF),  
Hussein Mwamba, majira ya saa 8:00 mchana
   (Shaffihdauda.blogspot)
 
 
No comments:
Post a Comment